HATIMAE GAMBA LA NYOKA KUJIVUA MAGAMBA

11:31 AM tibazetuasili 0 Comments


"Hakuna Mgumu kwenye mapenzi"na hakuna awezaye kushinda na Asili ( Nature) Men are born to marry an women to be married" Mwenyekiti wa Katiba wa Azaniaalumni2000 Twahil Abbas ama almaharufu GAMBA LA NYOKA hatimae amekubali yaishe kwa kuamua kujivua magamba na kuliacha kundi la makapera likipata pigo kubwa lisilo mfano kwa kufunga ndoa na mchumba wake kipenzi.

Kwa habari zilizo rasmi na zisizo na chembe hata kidogo ya chumvi kutoka chanzo cha kuaminika cha Mwenyekiti huyo wa rasimu ya katiba na pia yeye Mwenyewe ndoa hiyo inatarajiwa kufungwa visiwani Zanzibar Mwishoni mwa mwezi wa 5/16 na kufuatiwa na sherehe kubwa katika sehemu maalumu iliyoandaliwa PORT VIEW Hotel yenye maanzali mwanana ukanda wa juu kusini mwa Zanzibar .

Ukiwa Mtu wa karibu wa Twahil Abbas unaombwa kushiriki kwa hali na mali ili kufanikisha shughuli hii, maelezo ya ufanikishaji wa shughuli hiyo tazama maelezo katika kivuli cha kadi. 
Familia ya Azaniaalumni2000 inamtakia kila la kheri Ndugu Twahil Abbas ama Gamba la Nyoka katika tukio hilo muhimu maishani.

You Might Also Like

0 comments: