michezo

BONANZA LA WATANI WA JADI SIMBA NA YANGA LANUKIA

2:06 AM tibazetuasili 1 Comments


Hayawi hayawi sasa yamekuwa ule mpambano wa soka kati ya mashabiki wa Simba na Yanga kutoka Azapound Family umeiva, baada ya tambo zinazoendelea kuzidi na kupelekea ubishi huo kwenda kuamulia uwanjani. Mashabiki hao wa timu mbili wamemuomba Mwenyekiti wa AzaniaAlumni Ndugu Mwinyi Hassani kuandaa mpambano huo kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kumaliza ubishi huo.




Mpaka sasa tayari wameshajitokeza baadhi ya member wakithibitisha ushiriki wao katika mtanange huo, Diaz Batholomeo yeye amesema yeye atawakilisha upande wa Yanga kama Golikipa na Omar yeye amesema yupo neutral ni mchezaji huru upande wowote ukimuhitaji atauchezea.

Kwa upande wa wanazi wa Yanga wakiongozwa na Katibu wa Azananiaalumni2000 ndugu Simoni Matere wamemwambia Diaz licha ya kuonyesha mapenzi yake kwa Mabingwa hao wa Bara msimu huu hawatakuwa tayari kumruhusu kukaa golini kwani imeonekana ni mamluki wa Simba anayetaka kuipa ushindi timu yake kijanja, na kumtaka akae mbali kabisa na kama ikiwezekana aende kuungana na mashabiki wenzie kuomboleza msiba wa timu yake, kwa kukosa ubingwa na kuendelea kubakia kushiriki makombe ya Mbuzi ( Mchangani ).

Ama kwa hakika terehe hiyo inasubiliwa kwa hamu kubwa sana ili kuona ni nani atakaye ibuka mshindi siku hiyo.

You Might Also Like

1 comment: