jamii

HONGERA NTIMI OMEGA MWAKIPAKE KWA KUFUNGUA UKARASA MPYA

4:14 AM tibazetuasili 1 Comments


"Mungu Mkubwa" ndio neno pekee lifaalo kwa kuanza nalo,lile tukio muhimu lililokuwa likisubiliwa kwa hamu hatimaye limetimia usiku wa tarehe 25 Jul 2015 katika Hotel ya Double Tree, Mwana Azapound Ntimi Omega alifanikiwa kufungua ukurasa mpya wa maisha baada ya kukamilisha tukio muhimu la kufunga pingu za maisha na mahabuba wake Bi Apaisaria Derreck.Ilikuwa ni siku ya faraja kwa familia nzima na watu wakaribu yake bila kusahau Azapound for life.Pongezi nyingi sana ziwaendee azaniaalumni2000 wote waliojitokeza katika tukio hilo muhimu na kuweza kumpa faraja mwana familia mwenzetu ama kwa hakika azaniaalumni2000 we show greats support to our fellow, there is nothing word could explain this expect big up for those whose take time to participate at the wedding.
Mahaba niue!!!! Mr Ntimi Mwakipake akimuweka shera vizuri Mkewe Mrs Apaisaria Mwakipake 

Pongezi pia ziwaendee viongozi wa azaniaalumni2000 wote kwa moyo wao wakuhamasisha katika kipindi chote cha matukio.Azapound inawatakiwa kila la kheri Mr na Mrs Ntimi familia yenye furaha tele maishani.


Mr & Mrs Ntimi wakitembea kwa pozi kutoka kanisani mara baada ya kuapa kiapo cha kuishi kwa raha na shida katika siku za maisha yao.



Mwenyekiti wa azaniaalumni2000 Ndugu Mwinyi Hassani akitoa salam na pongezi kwa bibi Harusi,azapound walipokuwa wakiwasili 

 Furaha ya kweli haiwezi kujificha...Bwana Harusi Ntimi Omega akiikalibisha familia yake ya azapound ili ijumuike naye katika siku yake maalumu

 Nuhu Magwai much respect

 Mzee wa Tumbaku ( Mwalami Kwengwegu )  uwepo wako umeheshimika

  Welcome Masoud Shakur azaniaalumni2000 blogger!!!!!!!!!

 Welcome Mzee wa Kamati ya Jamii Man Costa 

Mwenyekiti karibu sana

Ikafika muda wa kila mmoja kukamata kinywaji mkononi nakuwatakia  baraka tele Bwana na Bibi harusi...ni mwendo wa Cheers tu!!!!!

 Cheers Maprosooooo

 Tumekukamata huna pakwenda,Tugonge Cheers huku tukipiga funda moja moja 





Cheers ziligongwa sana na story za hapa na pale ziliendelea 

Bwana Harusi akawa hoi, nakutuambia niacheni nikakae kulee mbele nanyi kaaeni mnywe na mtulie

 Mwenyekiti Azaniaalumni alihakikisha hakuna kitu kinampita hata kama kinatokea kwa mbali

 Husband and Wife wakiteta jambo na Bwana Nuhu Magwai

Man costa, Steve na Ommy Pengo wakiwa katika pozi tofauti, all in all waliwakilisha azapound vyema 

  Masoud Shakur akifurahi jambo na Bwana Maprosoo

Vinywaji  tele ndani ya glass vikiisha sema uletewe,ndio ilikuwa slogan

 Muda wa Maakuli ukafika,kuku kubanika ,kuku roast, samaki wa kuoka ,nyama karanga roast, mapokopoko njani,mantarashushi na madabiz dabizi masetojo ,saladi vitunguu,mayonaizi pilipili sagwa, pondwa na kuchemsha kila aina ya flava,acha tu

Mwenyekiti katika ubora wake

Session ya manywaji na chakula ikaaisha,ikafika zamu ya azapound kupewa jukwaa na kucheza kwaito,cheza kwa step usimkanyage mwenzio

Step bin step usimkanye mwenzio

kama ingetokea humfahamu katibu wa azaniaalumni2000 na ukaambiwa ndio huyu bila shaka ungesita kuamini,kwaito iliomba poo

Huu si muda wa ukada ni muda wa kwaito step kwa step ni kama maneno haya yalikuwa yakimtoka Nyakia ally vile

twende kushoto tatu rudi kulia tatu,step kwa step 


 Punguza spidi watu bado wanashibe,Bwana Harusi akimtaahadhalisha Mwenyekiti

Music Session is End, ila inaonekana bado wana wa Azapound walikuwa na Ugwadu vibaya sana

Session ya kuwaaga na kuwatakiwa  Bwana na Bibi harusi kila la kheri katika maisha yao mpya ikiwadia
















Azaniaalumni2000 inamtakia kila la kheri Ndugu Ntimi Mwakipake na Mkewe Bi Apaisaria Derreck Mungu awape afya njema na familia yenye furaha na amani, pia pongezi kubwa ziwaandee azapound wote kwa kushiriki kwa namna moja au ingine katika kufanikisha shughuli hiyo.









!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


You Might Also Like

1 comment: