Afya

LIJUE STAFELI TUNDA LENYE UWEZO WA KUPAMBANA NA SARATANI

1:00 PM tibazetuasili 0 Comments



Stafeli ama topetope ni tunda  linalopatikana katika mikoa ya Morogoro, Iringa Tanga, Mbeya, na baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam. 


Tunda hili linaelezwa kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali ikiwamo saratani, unaweza kulila tunda hili kama lilivyo au kutengeneza juice yake vyote uleta matokeo chanya.



USHAHIDI WA KIMAABARA

Kwa mujibu wa Jarida la Kemia na madawa la nchini Marekani la mwaka 2010 linaeleza kuwa tunda hili la Stafeli au Mtopetope kuwa lina uwezo wa kuangamiza chembe hai zenye saratani pasipo kuleta madhara katika mwili. 



Taasisi ya utafiti wa Saratani ya Nchini Uingereza (NIR) ilifanya utafiti wa kwanza kuhusu maajabu ya stafeli mwaka 1976 na kubaini kuwa majani, mizizi na tunda la stafeli, vyote vina uwezo wa kutibu saratani. 




Ingawa suala la Stafeli peke yake kutibu saratani lina mjadala lakini kutokana na majaribio zaidi ya 20 yaliofanywa yamebaini stafeli lina virutubisho vyenye uwezo wa kupambana na kupunguza makali ya saratani. Pia majaribio hayo yamebaini stafeli huua chembechembe za saratani aina 12 (cancerous cell ) ikiwemo saratani ya Matiti, Mapafu, kongosho, kibofu na tumbo.


kansa ya titi

 kansa ya Pafu

  
Kansa ya Tumbo
Stafeli lina mchanganyiko wa virutubisho wenye uwezo mkubwa wa kuthibiti  ukuwaji wa seli  za saratan mara 10,000 zaidi ya dawa ya adriamycin ambayo ndio hutumika kutibu saratani. 

              
mchanganyiko wa virutubisho vya Annonaceous na Acetogenins vilivyomo kwenye stafeli huua seli zilizoathirika na saratani tu tofauti na dawa za kisasa ambazo huua seli zilizoathirika na zisizoathirika.
Stafeli uthibiti ukuwaji wa seli za saratani bila kusababisha madhara mengine tofauti na ilivyo kwa dawa za kisasa ambazo uleta madhara kiafya kwa mgonjwa pindi atumiapo iwe zile za mionzi, sindano au vidonge.
Mwana Azaniaalumni2000 pendelea kula tunda hili mara kwa mara ili kujikinga na kunyemelewa kwa ugonjwa huu ambao umekuwa hatari dunia kwasasa.
 

♣♣♣♣♣♣♦♦♦♦♦♦♦♥♥♥♥♥ ©copyright masoud shakur

You Might Also Like

0 comments: