jamii

NIMEKULETEA RASIMU YA KATIBA PENDEKEZWA YA AZANIA ALUMNI 2000

10:16 AM tibazetuasili 0 Comments




KATIBA YA CHAMA CHA AZANIA ALUMNI 2000

SEHEMU YA I: UTANGULIZI

IBARA 1: Utangulizi:

Kwakuwa:
Maendeleo ya watu katika jumuiya au Taifa lolote hutegemea ufahamu wa namna bora ya kutumia rasilimali zilizopo;
Na kwa kuwa:
Umoja wa watu hao na ushirikiano kati yao kwa njia ya kufahamiana, kusaidiana ni muhimu kwa ujenzi wa ufahamu huo;Jukumu la kuleta maendeleo ya wanajamii wa AZANIA ALUMNI 2000 ni la wanajamii wenyewe kwa njia ya kuunganisha nguvu, juhudi na maarifa yao na jamii  na mamlaka nyinginezo;
Na kwa kuwa:
Wameunganishwa na Umoja wao wa AZANIA ALUMNI 2000 wanachama wana jukumu la kusaidiana na kushirikiana.

Kwa hiyo basi:
Kwa pamoja tunaungana na kukubaliana yafuatayo:

SEHEMU YA II: DIRA, DHAMIRA NA MADHUMUNI

IBARA 2: Dira

Kuwa Chama bora kinachohamasisha Umoja na uelewano na chenye uwezo wa kuwawezesha wanachama wake na jamii inayokizunguka kiuchumi na kijamii
IBARA 3: Dhamira

Kuchangia na kuleta ushirikiano wa kijamii ili kuinua kiwango cha maisha ya wanachama kwa kuwezeshana kama wadau ndani na nje ya Chama

IBARA 4: Madhumuni Ya Kuanzisha Chama

(i)           Kushirikiana katika taabu na raha kama vile Sherehe, Ugonjwa na Misiba
(ii)         Kukuza uwezo wa Chama kwa  kuanzisha shughuli za kimaendeleo na biashara
(iii)         Kushirikiana na serikali na taasisi nyingine ndani na nje ya nchi zitakazofaa kutimiza malengo ya Chama chetu na kupokea toka serikalini haki na misaada mbalimbali ikiwemo kuomba, kununua au kukodi majengo au ardhi ya kufanyia kazi na rasilimali nyinginezo muhimu
(iv)      Kusaidia vikundi vya kijamii vyenye uhitaji maalum.
(v)        Kuhamasisha na kuwezesha shughuli za michezo kwa wanachama

SEHEMU YA III: KATIBA, USAJILI NA ENEO LA UTENDAJI KAZI

IBARA 5: Matumizi ya Katiba
Katiba hii itatumika kwa malengo yaliyokubaliwa na wanachama wake na kuongozwa kwa kanuni zake.
Katiba hii itaanza kutumika mara baada ya kupitishwa na wanachama kwa asilimia zaidi ya hamsini.
 
IBARA 6: Jina La Chama
(i)           Jina la chama litakuwa AZANIA ALUMN 2000
(ii)         Na kifupi chake kitakuwa (AA2000)

IBARA 7: Usajili
Chama kitasajiliwa kwenye mamlaka husika mara itakapoamuliwa na mkutano mkuu wa wanachama
                                 
IBARA 8: Ofisi Kuu
Makao makuu ya Chama yatakuwa Dar es Salaam.
                         
IBARA 9: Eneo La Utendaji Kazi
Chama kitafanya kazi Tanzania na nje ya mipaka yake

SEHEMU YA IV: UANACHAMA NA AINA ZA WANACHAMA
IBARA 10: Sifa za Mwanachama
(i)     Awe mwanafunzi aliyemaliza masomo ya sekondari yaani Ordinary Level mwaka 2000 katika shule ya sekondari Azania.
(ii)         Awe na akili timamu na mwenye kutimiza majukumu yake ya kufanya kazi za Chama.
(iii)        Awe ameingia kwenye chama kwa hiari yake mwenyewe bila kushurutishwa na mtu yeyote yule.
(iv)      Awe analipa ada na michango ya Chama kama itakavyopendekezwa na Chama.
(v)        Mwana Azania 2000 atakayeomba kujiunga baada ya Chama kuanzishwa, ada yake ya kiingilio itategemea na kiwango kitakachopitishwa na mkutano mkuu, sambamba na maombi yake kujadiliwa na mkutano huo.

IBARA YA 11: Haki za Mwanachama

a.     Kupata taarifa za shughuli za Chama kwa kufuata taratibu
b.     Kuchangia mawazo, fikra na maoni mbalimbali katika Chama
c.     Kuchagua au kuchaguliwa kushika nafasi mbali mbali za uongozi
d.     Kufanya kazi za Chama kama zinavyomhusu
e.     Kuhudhuria vikao na mikutano  ya Chama inayomhusu
f.        Kuwa tayari kupambana na aina yoyote ya uonevu, ukandamizaji udhalilishaji na ubaguzi ndani ya Chama kwa kuzingatia sheria za nchi
g.     Kujitetea, kusikilizwa, kuheshimiwa na kukata rufaa anaposhitakiwa ama kuchukuliwa hatua za kinidhamu ndani ya Chama
h.     Kila Mwanachama anayo haki ya kuchangiwa kwenye msiba, sherehe, magonjwa au tatizo lolote ambalo kamati ya jamii na sekretarieti ya chama itaona umuhimu wake.
i.         Mwanachama anayo haki ya kujitoa na stahiki zake atazipata kutegemeana na kanuni zilizopo na sababu zake za kujitoa. Mwanachama atakayejitoa au kufukuzwa kwenye chama atakuwa amepoteza stahiki zake zote.
j.         Mwanachama atataja jina la Mrithi wake na anaweza kubadili jina la Mrithi wake wakati wowote, Mrithi atakuwa na haki zote za marehemu isipokuwa haki ya uanachama
k.      Mwanachama ana haki ya kupata haki sawa na wanachama wengine

IBARA YA 12: Ukomo wa Uanachama
(i)           Kutokana na mwenendo usioendana na madhumuni , kanuni za maadili na  sera za chama
(ii)          Kujitoa  AZANIA alumni  kwa hiari yake mwenyewe
(iii)        Kutolipa ada na michango ya chama kwamuda wamiezi mitano mfulilizo
(iv)       Kuugua ugonjwa wa akili baada ya kuthibitishwa na daktari utakaopelekea kushindwa kutimiza wajibu wake wa uanachama.
(v)        Kushindwa kuhudhuria mikutano ya chama au vikao bila ya sababu ya kuridhisha kwa kipindi cha miezi kumi na miwili mfululizo
(vi)       Mwanachama akishindwa kuhudhuria mikutano mikuu mitatu mfululizo bila taarifa rasmi
IBARA YA 13: Wajibu wa Mwanachama.                                            
(i)           Kujadili na kupitisha mipango ya shughuli zinazohusu chama
(ii)         Kujadili, kuthibitisha na kupitisha mapato na matumizi ya chama
(iii)        Kujadili nidhamu ya wanachama na katika kupendekeza hatua za kuchukua
(iv)      Kufanya shughuli za chama kama inavyompasa.
(v)        Kuchangia gharama za uendeshaji chama kwanjia za ada na michango iliyoamuliwa na chama
(vi)      Kuwa tayari kupambana na aina yeyote ya uonevu, ukandamizaji, udhalilishaji na ubaguzi ndani ya chama kwa kuzingatia sheria za nchi.
(vii)     Hakuna mwanachama mwenye nafasi yakuridhia au kutoa wazo la kuvunjika kwa umoja huu.
(viii)   Kulinda na kutetea katiba halali ya Azania Alumni 2000 iliyopitishwa na wanachama katika mkutano mkuu.

    SEHEMU YA V SIFA NA MUUNDO WA UONGOZI
IBARA YA 14:  Sifa za Uongozi
(i)              Awe mwanachama aliyelipa michango ya chama kwa muda wamiezi mitatu(3) mfululizo
(ii)            Asiwe mwenyekiti au kiongozi wa chama chochote ambacho kitaathiri shughuli za chama.
(iii)           Awe anajua kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili
(iv)         Awe mwanachama kwa muda wamiezi 12
(v)           Awe na upeo wa kuchambua, kujadili masuala ya chama na maendeleo yake
(vi)         Awe mwaminifu, mwenye moyo wa kujitolea nakupenda kupokea ushauri kwa wenzake
(vii)        Kiongozi anatakiwa mwenye afya njema ya kumuwezesha kusoma, kuandika na kusimamia shughuliza chama
(viii)      Awe mwaminifu, mwenye kujitolea na kupokea mawazo ya wenzake
(ix)          Asiwe amewahi kufukuzwa uanachama kwa makosa ya hujuma, ubadhirifu, wizi na mali ya chama.

IBARA YA 15: Sekratariat
Kutakuwa na chombo cha juu cha uongozi kitakachojulikana kama Sekratariat kitakachoundwa na viongozi wafuatao
(i)                 Mwenyekiti
(ii)                Makamu Mwenyekiti
(iii)               Katibu
(iv)             Naibu Katibu
(v)              Mweka Hazina


IBARA YA 16: Mweyekiti
Kutakuwa na mwenyekiti atakayechaguliwa kwa wingi wa kura katika mkutano mkuu wa chama
IBARA YA 17: Majukumu ya Mwenyekiti
(i)           Mwenyekiti ndio kiongozi mkuu wa chama
(ii)         Mwenyekiti wa mikutano mikuu ya chama isipokuwa mikutano ya kamati.
(iii)        Kuitisha mikutano kwa kuzingatia katiba na kalenda ya chama kwa kusaidiwa na Katibu Mkuu
(iv)      Kuitisha mikutano ya dharura
(v)        Mlinzi na msimamizi mkuu wa katiba
(vi)      Atasaini mikataba yote iliyoridhiwa na chama
(vii)     Msemaji mkuu washughuli na maamuzi mbalimbali ya chama.
(viii)   Msimamizi na mfuatiliaji wa utekelezaji maazimio ya chama

YA 18: Makamu Mwenyekiti
          Kutakuwa na makamu mwenyekiti atakayepigiwa kura kwa nafasi ya mgombea mwenza.

YA 19: Majukumu ya Makamu Mwenyekiti
Kukaimu shughuli za mikutano kwa niaba ya mwenyekiti wakati mwenyekiti hayupo.
IBARA YA 20:  Katibu Mkuu
(i)           Mratibu na mtendaji mkuu wa shughuli za chama ikiwemo kuandaa mipango mbalimbali ya maendeleo ya chama
(ii)         Kuandaa na kutunza taarifa mbalimbali za shughuli za chama
(iii)        Kutakuwa na katibu mkuu wachama atakayepatikana kwa kupigiwa kura kwenye  uchaguzi mkuu wachama
IBARA YA 21:  Naibu Katibu Mkuu
Kutakuwa na Naibu Katibu Mkuu ambaye kazi yake itakuwa ni kukaimu shughuli za Katibu Mkuu
   
IBARA YA 22: Mweka Hazina
Kutakuwa na mweka hazina mwenye taaluma ya uhasibu ambaye shughuli zale zitakuwa kama ifuatavyo
1.         Kutunza kumbukumbu zote za fedha za Chama
2.         Kuhakikisha kuwa fedgha za chama zinatolewa kwa kuzingatia taratibu za fedha na katiba
3.         Msimamizi mkuu wa ukusanyaji wa michango, ada na mapato mengineyo ya chama kwa kufuata taratibu za chama.
4.         Kuandaa na kutoa taarifa za mapato na matumizi ya chama kwenye vikao vya chama,Mkutano Mkuu na pale zitakapohitajika.
IBARA YA 23: Ukomo wa Uongozi
1.      Viongozi wote wa Sekratariat watadumu madarakani kwa muda wa miaka miwili baada ya kuchaguliwa na wanaweza kugombea tena kuchaguliwa kwa vipindi vingine baada ya hapo.
2.      Viongozi wote wa Sekratariat watachaguliwa na mkutano mkuu wa chama kwa wingi wa kura.
3.      Uongozi uliopo madarakani utatakiwa kukabidhi madaraka na ofisi za chama wiki mbili baada ya uongozi mpya kuchaguliwa
4.      Madaraka ya kiongozi yeyote yatakoma iwapo kiongozi huyo atapoteza sifa za uongozi kwa mujibu wa ibara ya 14.
5.      Kujiuzulu
6.      Kuondolewa
7.      Kifo
8.      Kushindwa kutimiza majukumu yake kikatiba
9.      Kufutwa uanachama

 IBARA YA 24: Kiongozi Kuondoka Kabla ya Muda Wake
(i)        Ikiwa mwenyekiti au katibu  ataachia madaraka kabla ya muda wa uchaguzi, makamu wake atashilikia nafasi hiyo moja kwa moja. Sekretarieti itamteua mwanachama yeyote anayefaa kushika nafasi ya makamu ambae atathibitishwa na mkutano wa wanachama unaofuata kwa wingi wa kura. Ikiwa wanachama hawataridhika na uteuzi huo, wanachama watapendekeza majina matatu kisha kupigiwa kura. Mshindi atapatikana kwa kupata kura nyingi.
(ii)      Bila ya kuathiri Ibara ya 20 , Ikiwa mweka hazina ataachia madaraka kabla ya muda wa Uchaguzi basi Sekratariat itamteua mwanachama yeyote anayefaa kushika nafasi nafasi inayofuata na atathibitishwa na mkutano wa wanachama unaofuata kwa wingi wa kura. . Ikiwa wanachama hawataridhika na uteuzi huo, wanachama watapendekeza majina matatu kisha kupigiwa kura. Mshindi atapatikana kwa kupata kura nyingi.
IBARA YA 25: KUKASIMU MADARAKA
Iwapo Mwenyekiti hayupo, majukumu yake yatachukuliwa na Makamu Mwenyekiti, Iwapo Makamu Mwenyekiti hayupo madaraka yatachukuliwa na Katibu, Iwapo Katibu hayupo Madaraka yatachukuliwa na Naibu Katibu.

SEHEMU YA VI: MIKUTANO
IBARA 26: Mkutano Mkuu wa Mwaka
Kutakuwa na mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wote utakaofanyika kulingana na kalenda ya chama ili kupitisha maazimio na mambo mengineyo kama yalivyoelezwa katika katiba hii kwa mwaka husika
IBARA 27: Mkutano Mkuu wa dharura
(i)           Kutakuwa na mkutano maalum wa dharura kulingana na ulazima wa kufanya hivyo , na wanachama wote wanapaswa kuhudhuria.
(ii)         Mwenyekiti kwa kushirikiana na Sekratariati anaweza kuitisha mkutano mkuu wa dharura kama kuna ulazima wa kufanya hivyo wakati wowote
(iii)        Mwanachama anaweza kuomba kuitishwa kwa mkutano mkuu wa dharura kujadili jambo lolote linalohusu chama iwapo atapata uungwaji mkono wa asilimia hamsini za wanachama wote kwa majina yao na saini zao, Mwenyekiti atalazimika kuitisha Mkutano huo wa dharura ndani ya muda wa siku 14 baada ya madai hayo kuwasilishwa kwa katibu wa sekratariati na nakala kuwasilishwa kwa kamati ya maadili na mashauriano.

IBARA 28: Mikutano ya Kawaida
Kutakuwa na mikutano ya kawaida itakayofanyika kila baada ya miezi minne ya mwaka kwa vipindi vitatu kwa wanachama wote kujadili utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa kwenye mkutano mkuu na masuala mengineyo ya chama.

IBARA YA 29: Wajumbe wa Mkutano Mkuu
i.           Wajumbe wa mkutano mkuu watakuwa wanachama wote waliotimiza masharti    yote kwa mujibu wa Ibara ya 13 ya sifa za mwanachama
ii.         Ili mkutano mkuu uwe halali, ni sharti uhudhuriwe angalau kuanzia theluthi ya wanachama wote

IBARA YA 30: Wajibu, Mamlaka, na Kazi za Mkutano Mkuu
                                   i.            Kujadili na kupitisha mipango ya shughuli za mwaka za Chama.
                                 ii.            Kujadili, Kuthibitisha na kupitisha mapato na matumizi ya Chama ya mwaka unaofuata
                               iii.            Kupokea, kujadili na kutolea mmaumuzi taarifa mbalimbali zinazowasilishwa na kamati mbalimbali za Chama
                               iv.            Kurekebisha katiba.
                                 v.            Kupokea taarifa mbalimbali za kamati
                               vi.            Kuchagua viongozi wa kusimamia chama katika nafasi zilizowekwa kwa mujibu wa katiba hii na zile zitakazotokana na shughuli za chama kuongezeka
                             vii.            Kupokea, kujadili na kutolea maamuzi ada ya kila mwezi ya kila mwanachama baada ya kupokea mapendekezo kutoka kwa wanachama


IBARA 31: Kukasimu Madaraka ya Mkutano Mkuu
Nafasi ya Mwenyekiti na katibu inaweza kukasimiwa kwa mwanachama yeyote atakaechaguliwa na wanachama ili kuendesha mkutano mkuu iwapo kutakuwa na haja ya kufanya hivyo.

SEHEMU YA VII: VYANZO VYA FEDHA, UTUNZAJI NA MATUMIZI YAKE
IBARA 32: Vyanzo vya Fedha
i.                  Viingilio, ada na michango ya hiari ya wanachama
ii.                Fedha kutoka taasisi zinazokopesha kama itakavyoidhinishwa na wanachama
iii.             Michango ya hiari ya wahisani, wadau wa maendeleo ndani na nje ya nchi
iv.             Michango ya hiari toka kwa mashirika na watu binafsi
v.               Harambee halali
vi.             Miradi mbalimbali ya Chama
vii.           Tozo kutokana na adhabu mbalimbali

IBARA 33:     Mwaka wa Fedha na Matumizi ya Fedha za Chama
Kutakuwa na mwaka wa fedha wa Chama utakaokuwa unaanza mwezi Januari na kuishia Desemba.

IBARA 34:     Matumizi ya Fedha za Chama
i.               Kuendesha miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuinua kipato cha chama na wanachama .
ii.             Kulipia gharama mbalimbali  za uendeshaji wa shughuli za chama .
iii.            Kusaidia jami hitaji kama itakavyopendekezwa na kuamuliwa na chama
iv.          Kusaidia wananchama katika misiba , sherehe, ugonjwa au tatizo lolote ambalo chama kitaridhia.

IBARA 35:     Uendeshaji wa Akaunti za Benki
Chama kitakuwa na akaunti katika benki zinazotambulika kisheria

i.                  Kutakuwa na watia saini wanne katika akaunti hizo, ambao wamewekwa katika makundi wawili:

KUNDI A.
1.               Mwenyekiti
2.               Mweka Hazina

KUNDI B.
3.               Mwenyekiti au Katibu wa Kamati ya Uchumi
4.               Mjumbe Mmoja atakayeteuliwa katika Mkutano Mkuu



ii.                Ili kuruhusu fedha kutoka katika akaunti hizo kutumika kwa mujibu wa matumizi yaliyoainishwa kwa mujibu wa katiba hii sharti saini mbili za kati ya watia saini hao wanne waliodhinishwa ziwepo  na ya mwenyekiti ikiwa ni ya lazima.

IBARA 36:     Taarifa za Fedha
i.                     Taarifa ya fedha itakuwa inatolewa kwa wanachama wote kwenye mikutano yote ya kila baada ya miezi mine, Mkutano Mkuu na pale itakapohitajika.
ii.                   Taarifa itayarishwe na kuwafikia wanachama wiki moja kabla ya mkutano husika ili kufanya uchambuzi na kujitayarisha na mkutano.
iii.                  Taarifa ya fedha ya mwisho wa mwaka inatakiwa iwe imekaguliwa na mkaguzi wa mahesabu kutoka nje ya chama ( external auditor)

IBARA 37:     Ukaguzi wa Fedha
i.                     Ukaguzi wa mapato na matumizi ya fedha za chama utafanyika mara moja kwa mwaka
ii.                   Ukaguzi maalumu wa mapato na matumizi ya fedha za chama utafanyika wakati wowote pale utakapohitajika
iii.                  Uongozi utawasilisha ripoti ya ukaguzi ya mapato na matumizi ya chama kwa wanachama kwenye mkutano mkuu

SEHEMU YA VIII:     MABADILIKO YA KATIBA NA LAKIRI

IBARA 38:     Mabadiliko ya Katiba
Katiba hii inaweza kubadilishwa na mkutano mkuu wa wanachama wa mwaka au mkutano mkuu maalum. Marekebisho yanaweza kuletwa na mwanachama na kuungwa mkono na kupigiwa kura na wanachama kwa wingi wa theluthi mbili au zaidi.



IBARA 39: Mhuri au Lakiri ya Chama
Chama kitakuwa na Muhuri au lakiri yenye jina la Azania Alumni 2000. Mhuri au Lakiri ya Chama haitatumika popote isipokuwa kwa idhini na mamlaka ya Mwenyekiti na Katibu mkuu au kiongozi anayekaimu nafasi hizo.


SEHEMU YA IX: KAMATI  ZA CHAMA
IBARA YA 40: Kutakuwa na kamati za chama zifuatazo
1.         Uchumi na Mipango
2.         Mambo ya jamii
3.         Maadili na mashauriano
4.         Rufaa
Wajumbe wa kamati hizi idadi yao haitapungua watu wanane

IBARA YA 41: MAJUKUMU YA KAMATI
1.    Kamati ya mipango na Uchumi
i.                     Kutafiti, kupembua miradi mbalimbali ya chama.
ii.                   kuanzisha na kusimamia miradi ya chama kwa ridhaa ya wanachama.
iii.                  Kutoa taarifa za miradi kwa Uongozi na wanachama pale itakapohitajika
iv.                Kuhakiki na kutunza taarifa za miradi ya chama
v.                  Kushauri chama kuhusu miradi mbalimbali

2.    Kamati ya maadili, mahusiano na mashauriano
i.                  Kupokea, kusikilza na kutolea maamuzi migogoro yote inayoathiri utendaji wa chama
ii.                Migogoro binafsi pia inaweza kutatuliwa na kamati hii
iii.               Kuchunguza na kupendekeza hatua za kuchukua dhidi ya kiongozi yeyote na mwanachama kwa makosa mbalimbali yanayo athiri au yatakayo athiri heshima, taswira na utendaji wa chama.

3.    Kamati ya jamii
i.                  Kuratibu na kushughulikia masuala yote ya kijamii kama misiba, sherehe na matukio mbalimbali ya wanachama
ii.                Kuratibu matukio yote yenye lengo la kujenga na kuimarisha urafiki, mshikamano na undugu baina ya wanachama.
iii.               Kutoa taarifa na kushiriki kikamilifu kwenye shughuli mbalimbali za chama
iv.             Kutoa ushauri kwa sekretarieti na wanachama kuhusu masuala ya jamii
v.               Kamati ya maadili, mahusiano na mashauriano itaweza kumuita mtu yeyote ndani ya chama kutoa ushahidi, maelezo au taarifa zozote zitakazosaidia utendaji wa kamati.
vi.             Iwapo migogoro binafsi isiyohusu Chama baina ya wanachama kwa ridhaa zao itatolewa maamuzi  na kamati hii, Iwapo yeyote katika wale wenye Mgogoro hawataridhika na hukumu yake, basi hawana nafasi ya kukata rufaa katika kamati ya rufaa.
4.    Kamati ya rufaa
(i)           Kupitia na kutolea maamuzi rufaa zote za masuala yanayohusu Chama.

(ii)         Kamati ya rufaa itaweza kumuita mtu yeyote ndani ya chama kutoa ushahidi, maelezo au taarifa zozote zitakazosaidia utendaji wa kamati.

IBARA YA 42: Wajumbe wa Kamati za Chama
(i)           Kamati ya Rufaa itaundwa na Wajumbe huru watakaotoka miongoni mwa Wanachama wote
(ii)         Kamati ya Maadili na Mashauriano itaundwa na Mkutano Mkuu kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao siyo viongozi na wala wajumbe katika kamati nyingine yoyote  katika chama..
(iii)        Wajumbe wa Kamati za Mipango na Mambo ya Jamii watateuliwa na Mwenyekiti kwa kushauriana na Wajumbe wengine wa sekreterieti.



You Might Also Like

0 comments: